Sunday, January 17, 2016

Jedwali la msimamo wa ligi ya EPL



Nambari Klabu Mechi Mabao Alama
1 Arsenal 22 16 44
2 Leicester 22 13 44
3 Man City 22 22 43
4 Tottenham 22 20 39
5 Man Utd 22 8 37
6 West Ham 22 8 35
7 Stoke 22 2 33
8 Crystal Palace 22 -1 31
9 Liverpool 22 -3 31
10 Southampton 22 7 30
11 Everton 22 7 29
12 Watford 21 1 29
13 West Brom 22 -8 27
14 Chelsea 22 -3 25
15 Bournemouth 22 -11 24
16 Norwich 22 -14 23
17 Newcastle 22 -15 21
18 Swansea 21 -11 19
19 Sunderland 22 -18 18
20 Aston Villa 22 -20 12 

Rouhani apongeza makubaliano ya nyuklia

Rais Hassan Rouhani amesema Jumapili (17.01.2016) wale waliokuwa na mashaka ambao walionya makubaliano ya nyuklia na mataifa yenye nguvu hayatokuwa na manufaa kwa Iran "wote wamethibitishiwa kuwa walikuwa sio sahihi.
Rais Hassan Rouhani katika mkutano na waandishi wa habari Tehran. (Jumapili 17.01.2016) Rais Hassan Rouhani katika mkutano na waandishi wa habari Tehran. (Jumapili 17.01.2016)
Rouhani amewaambia waandishi wa habari mjini Tehran kwamba "masaa machache tu " baada ya kuanza kutekelezwa kwa makubaliano hayo ya nyuklia na kuondolewa kwa vikwazo "njia 1,000 za mikopo zimefunguliwa na benki mbali mbali."
Amesisitiza kwamba makubaliano hayo sasa yatarahisisha kampuni za Iran kufanya kazi baada ya kutengwa kwa miaka mingi katika mfumo wa fedha wa kimataifa.
Rais huyo amesema "leo tuko katika hali ambapo kwayo tunaweza kuwa na mawasiliano ya kisiasa,kiuchumi na kisheria na dunia kwa maslahi ya taifa."Ameongeza kusema "tunaamini umoja wetu wa kitaifa.Tunaamini mafanikio yetu ya taifa."
Aliuchezea kamari wadhifa
Rais Hassan Rouhani wa Iran. Rais Hassan Rouhani wa Iran.
Matamshi yake hayo yalikuwa ni jibu kwa wale waliokuwa na mashaka waliosema kwamba mafanikio hayo ya kidiplomasia ya makubaliano hayo ya nyuklia hayawezi kutafsiriwa kwa vitendo vya faida ya kiuchumi kwa uchumi wa nchi hiyo.
Rohani aliuchezea kamari wadhifa wake wa urais kwa mazungumzo hayo ya nyuklia kwa kuimarisha juhudi za kidiplomasia na zenye kuhusisha Uingereza,China, Urusi,Ufaransa, Marekani na Ujerumani baada ya kuingia madarakani hapo mwezi wa Augusti mwaka 2013.
Ni wiki iliopita tu amesema wananchi wa Iran wanapaswa kusubiri kwa hamu "mwaka wa neema" baada ya nchi hiyo kuondolewa vikwazo.
Saudi Arabia yakosolewa
Waziri wa Mambo ya nje wa Iran Mohammad Javad Zarif akishangiliwa bungeni kwa kufanikisha makubaliano ya nyuklia. Waziri wa Mambo ya nje wa Iran Mohammad Javad Zarif akishangiliwa bungeni kwa kufanikisha makubaliano ya nyuklia.
Rouhani pia amekosowa shutuma za Saudi Arabia kwa makubaliano hayo ya nyuklia kwa kumtaja afisa mmoja bila ya kulintangaza jina lake ambaye alisema kuondolewa kwa vikwazo ni hatua mbaya.
Akizungumzia hilo amesema "siku ya utekelezaji wa makubaliano hayo tumemuona afisa mmoja wa Saudia akielezea masikitiko yake kwamba matatizo ya kiuchumi ya Iran yamepatiwa ufumbuzi."
Amesema jirani hatakiwi kamwe kufanya hivyo.Muislamu hawezi kufanya hayo.Muislamu hatakiwi katu kukasirika kwa kufarajika kwa Muislamu mwenzake. Waislamu wote ni ndugu."
Hali ya mvutano
Wakati ubalozi wa Saudi Arabia ulipovamiwa Tehran. Wakati ubalozi wa Saudi Arabia ulipovamiwa Tehran.
Kufuatia hatua ya Saudi Arabia nchi ya ufalme wa Kisunni kutekeleza adhabu ya kifo kwa sheikh wa Kishia Nimr al Nimr hapo Januari pili ubalozi wa Saudi Arabia mjini Tehran ulivamiwa kitendo ambacho kililaaniwa na Rais Rouhani.
Siku moja kufuatia tukio hilo Saudi Arabia ilivunja uhusiano wake wa kibalozi na Iran.Rohani amesema mlango bado uko wazi kwa diplomasia lakini hauwezi kubakia wazi milele.
Amesema kile wanachotaka ni kutatua mizozo ya kanda hiyo kwa kutumia busara lakini wakati huo huo wananchi wao,serikali yao haitokubali hatua zisizo za kidiplomasia na zisizofaa.
Utekelezaji wa makuabaliano hayo ya nyuklia ya kihistoria kati ya Iran na mataifa yenye nguvu yanatarajiwa kufunguwa uhalisia mpya wa kiuchumi nchini Iran.
Zaidi ya dola bilioni 30 za mali za Iran zilizozuiliwa nchi za nje zitaachiliwa mara moja kwa serikali ya Iran.Jumla ya mali za Iran zilizozuiliwa nchi za nje ni dola bilioni 100.

SHUDATE

Iran yarejea katika jumuiya ya kimataifa baada ya kutengwa kwa muda mrefu

Mkataba baina ya Iran na mataifa makubwa sita umeanza kutekelezwa baada ya shirika la kudhibiti matumizi ya nyuklia duniani IAEA kuthibitisha kwamba Iran imezitimiza dhima zake juu ya mkataba huo
Waziri wa mambo ya nje wa Iran, Mohammad Javad Zarif mjini Vienna Waziri wa mambo ya nje wa Iran, Mohammad Javad Zarif mjini Vienna
Iran imeondolewa vikwazo na jumuiya ya kimataifa vilivyouathiri uchumi wa nchi hiyo kwa kiwango kikubwa na kwa muda mrefu. Lakini itahitaji kiasi cha dola nusu Trilioni ili kuurekebisha uchumi wake.
Umoja wa Ulaya na Marekani zimetangaza kuviondoa vikwazo dhidi ya Iran baada ya kuhakikishiwa na shirika la IAEA kwamba nchi hiyo imevitekeleza vipengele vyote vya mkataba wa kihistoria,juu ya mpango wake wa nyuklia iliotiliana saini na mataifa makubwa sita, pamoja na Umoja wa Ulaya, mnamo mwezi wa Julai mwaka uliopita.
Marekani imefahamisha kwamba Iran sasa itaweza kuzipata fedha zake, kiasi cha dola Bilioni 50 zinazotokana na mali zake zilizokuwa zinashikiliwa katika nchi za nje. Kwa mujibu wa taarifa, mali za Iran zilizokuwa zinashikiliwa katika nchi za nje zinafikia thamani ya dola Bilioni 100.
Hata hivyo nchi hiyo inahitaji kiasi cha dola nusu Trilioni ili kuurekebisha uchumi wake uliothiriwa kwa muda mrefu na vikwazo vya nchi za magharibi.
Busara, mdahalo na ushirikiano zaleta tija
Waziri Javad Zarif akizungumza na waandishi habari mjini Vienna Waziri Javad Zarif akizungumza na waandishi habari mjini Vienna
Waziri wa mambo ya nje wa Iran Mohammed Javad Zarif na Mkuu wa sera za nje wa Umoja wa Ulaya Federica Mogherini walithibitisha kuondolewa kwa vikwazo walipozungumza na waandishi wa habari katika mji mkuu wa Austria,Vienna.
Moghrerini amesema, kutokana na Iran kuitekeleza sehemu yake ya mkataba, vikwazo vya kimataifa, vya kiuchumi na vya kifedha vilivyowekwa na jumuiya ya kimataifa dhidi ya Iran vimeondolewa. Mkuu wa sera za nje wa Umoja wa Ulaya amesema makubaliano yaliyofikiwa na Iran ni imara na ya haki.
Muda mfupi baada ya mkutano na waandishi habari, Waziri wa mambo ya nje wa Marekani John Kerry naye alithibitisha kwamba Marekani pia imeviondoa vikwazo ilivyoweka dhidi ya Iran. Rais Barack Obama pia alitia saini agizo la kuzibatilisha hati juu ya kuiwekea Iran vikwazo.
Waziri wa mambo ya nje wa Iran Mohammad Javad Zarif amesema tarehe 16 ni siku nzuri kwa Iran,Mashariki ya Kati na kwa dunia nzima. Waziri Javad Zarif ameeleza kuwa kufanya mdahalo, kuheshimiana, na diplomasia ndiyo mambo yaliyoleta suluhisho, na siyo vitisho, vikwazo na mashinikizo.
Shirika la kudhibiti matumizi ya nishati ya nyuklia limesema wakaguzi wake walioenda nchini Iran waliweza kuthibitisha kwamba nchi hiyo imezitimiza dhima zake zote juu ya mkataba iliyoutia saini na mataifa makubwa sita pamoja na Umoja wa Ulaya.
Rais Iran Hassan Rouhani alitumia mtandao wa Twitter kusifu hatua ya kuiondolea nchi yake vikwazo.
Waziri wa mambo ya nje wa Uingereza Philip Hammond amesema hatua hiyo ya kihistoria italeta usalama zaidi duniani. Waziri Hammond ameeleza kwamba hatua ya kuanza kuyatekeleza makubaliano yaliyofikiwa na Iran , ambapo nchi yake Uingereza, pia ilitoa mchango mkubwa, itaifanya sehemu ya Mashariki ya Kati na dunia yote kwa jumla kuwa salama zaidi.
Ujerumani yapongeza kuondolewa vikwazo
Waziri wa mambo ya nje wa Ujerumani Frank-Walter Steinmeier amesema makubaliano na Iran ni mafanikio ya kihistoria kwa diplomasia.
Hata hivyo Seneta wa chama cha Demokratik nchini Marekani Richard Blumenthal ametaka Iran iwekewe vikwazo na Marekani kwa sababu ya kufanya majaribio ya makombora ya masafa marefu yanayokiuka maazimio ya Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa.
Wakati huo huo katika kile kinachozingatiwa kuwa ni kuanza kujengeka uhusiano mzuri baina ya Iran na Marekani nchi hizo zimebadilishana wafungwa.

SHUDATE