Thursday, October 26, 2017

PEMBEJEO BORA ZINAVYOWEZA KUCHOCHEA KILIMO BORA

Image result for kilimo bora                Image result for kilimo bora
KILIMO ni sekta inayotegemewa kiuchumi na Watanzania zaidi ya asilimia 75, kwa mujibu wa matokeo ya utafiti wa kitakwimu uliofanywa na mashirika tofauti ya ndani na kimataifa, Shirika la Chakula na Kilimo la Umoja wa Mataifa (FAO), kwa mujibu wa ripoti yake ya 2013, kilimo kinachangia asilimia 30 ya pato la ndani (GDP) na asilimia 64 ya pato linalotokana na mauzo nje ya nchi.
Kilimo ni sekta inatoa ajira mara 11 zaidi ya sekta nyingine za uzalishaji nchini, hivyo kuifanya kuwa na umuhimu wa pekee katika kukuza uchumi wa nchi na kustawisha maendeleo ya watu.
Ni kutokana na umuhimu huo, mwaka jana Baraza la Kilimo nchini (ACT) liliratibu utafiti uliojielekeza katika mifumo ya usimamizi kwa matumizi ya pembejeo za kilimo, mnyororo wa usambazaji na namna zinavyochochea uzalishaji kwa mkulima.
Utafiti huo uliofanywa na kampuni ya Match Maker Associates kwa niaba ya ACT, ulielekezwa katika mikoa yenye kanda zinazonufaika na mradi wa SAGCOT na Kaskazini mwa nchi.
Ofisa anayeshughulikia sera katika ACT, Laetitia William anasema utafiti huo ulifanyika kwenye wilaya tatu na kuzilenga pembejeo chache ambazo ni mbolea, mbegu na kemikali zinazotumika kwenye kilimo.
Wilaya hizo na mazao yaliyotumika katika utafiti huo kwenye mabano ni Mbozi na Babati (mahindi), Kilombero (mpunga), Babati (alizeti na maharage). Kwa mujibu wa ripoti ya Wizara ya Kilimo, mahitaji ya mbegu zilizoboreshwa nchini yanakadiriwa kuwa zaidi ya tani za ujazo 120,000 kwa mwaka wakati kiasi kinachosambazwa ni tani za ujazo 35,352 sawa na asilimia 59.
Hata hivyo, ripoti hiyo inaeleza kuwa matumizi ya mbegu hizo yapo kwa kiwango kidogo, ikikadiriwa kwamba asilimia 25 ya mazao yanayovunwa yanatokana na mbegu zilizoboreshwa wakati asilimia 75 ni kutoka kwenye mbegu za asili.
Hali hiyo inatokana na ukubwa wa bei inayotozwa kwa mbegu zilizoboreshwa, upatikanaji wake, miundombinu na mtandao duni katika usambazaji. Mtafiti John Alinanuswe kutoka Match Maker Associate Limited, anasema utafiti huo, pamoja na mambo mengine ulibaini kuwa kutokana na upatikanaji fedha usiokuwa wa uhakika kwa Taasisi ya Uthibitisho Rasmi Mbegu (TOSCI), wakati mwingine unasababisha kuchelewa kwa utekelezaji wa majukumu inayojipangia hususani kwenye ofisi zake zilizopo Arusha, Mwanza, Mtwara, Njombe na Morogoro.
Hali hiyo, kwa mujibu wa taarifa ya utafiti, imechangia pia sehemu ya ziara za ukaguzi wa TOSCI kukasimiwa kwa maofisa wa serikali ngazi ya wilaya. Alinanuswe anasema licha ya Kamati ya Taifa ya Mbegu (NSC) kuitisha mkutano wa wadau wa mbegu mara moja kwa mwaka, lengo likiwa ni kujadili masuala yanayohusiana na sekta hiyo, mahudhurio si ya kuridhisha kutokana na ushiriki kuwa suala la hiari.
Hata hivyo, ripoti hiyo inakosoa kwamba vikao hivyo vinaitishwa na kufanyika kitaifa wakati katika ngazi ya wilaya ufanisi wake ni mdogo na mara nyingi havifanyiki kutokana na sababu tofauti ikiwamo taasisi za wadau wa pembejeo za kilimo kutohudhuria.
Aidha, taarifa ya kitengo cha zana za kilimo katika Wizara ya Kilimo, inaonesha kuwa mahitaji ya mbolea yaliongezeka kutoka mita za ujazo 485,000 kwa msimu wa 2011/2011 kufikia 885,019 mwaka 2015/2016.
Mtafiti Alinanuswe anasema utafiti uliofanywa umebaini kuwa ubadilishanaji taarifa kati ya mamlaka zinazosimamia sekta ya kilimo nchini dhidi ya wadau wanaoshirikiana nao ni mdogo. “Katika majadiliano na mamlaka tofauti za usimamizi wa kilimo, hatukupata ushahidi wa kumbukumbu za pamoja za wadau wanaojihusisha na uingizaji na biashara ya pembejeo za kilimo,” anasema.
Hata hivyo, mwakilishi wa Tosci, Mtafiti Mwandamizi Doroth Ole Meiludi anasema hali hiyo imeboreshwa na kwamba miongoni mwa mamlaka hizo na hususani taasisi hiyo ya uthibitisho wa mbegu ina kumbukumbu hizo zinazosaidia kuleta ufanisi katika utekelezaji wa majukumu yao.
Lakini Alinanuswe anasema ukosefu wa kumbukumbu unasababisha ugumu katika kuisimamia sekta ya kilimo, kuwatambua wanaoshiriki vitendo viovu dhidi ya pembejeo na kuwachukulia hatua zinazostahili.
Anasema matokeo hayo yanaonesha kuwa mamlaka za usimamizi zinakabiliwa na upungufu wa rasilimali watu na fedha, akizitaja kuwa ni nyenzo muhimu zinazochochea ufanisi katika utoaji wa huduma kwa wakati.
Kuhusu mnyororo wa usambazaji pembejeo nchini, matokeo ya utafiti huo yanaonesha kuwapo kiwango duni cha uratibu wa pamoja wa shughuli za taasisi zinazoundwa na kampuni za uingizaji na biashara ya pembejeo.
Kampuni hizo zipo huru kujiunga na taasisi tofauti zilizoundwa ambazo ni pamoja na Chama cha Wafanyabiashara ya Mbegu (Tasta) na Chama cha Mawakala wa Mbegu (Tanada).
Alinanuswe anasema taasisi hizo zimebainika kupitia utafiti huo hazina uratibu wa pamoja na hakuna mfumo wa kuwezesha zikidhi sera na kanuni za mfumo wa usambazaji pembejeo nchini na kwamba hazijajiunda kusaidia shughuli za wasambazaji pembejeo kuwa na ufanisi.
Mtafiti huyo anasema stadi za utawala wa biashara kwa washiriki wengi wa pembejeo za kilimo hazipo kwa kiwango cha kuibua uwazi na ufanisi katika mfumo wa utoaji huduma husika.
Alinanuswe anasema ongezeko la matumizi sahihi ya pembejeo linaweza kuchangia kuongezeka uzalishaji na faida kwa wakulima. Utafiti unabaini kuwa sekta hiyo bado inakabiliwa na changamoto kadhaa zikiwamo ufinyu wa masoko, ubovu wa miundombinu, ukosefu wa taarifa sahihi, fedha na bima, hali inayoweza kufifisha ufanisi kwa wakulima, ikiwa hazitapatiwa ufumbuzi.
Wakati huo huo utafiti umebaini kiwango cha uwapo wa pembejeo bandia za kilimo kushuka kwa mwaka jana ikilinganishwa na ilivyokuwa mwaka 2012. Anasema watoa taarifa katika utafiti huo walieleza kuwa mbolea, mbegu na viuatilifu haziwaathiri kwa kiwango kinacholingana kama ilivyokuwa awali, akitoa mfano kada chache kama za watumishi katika halmashauri za wilaya na wakulima pekee, walizungumza uwapo wa mbolea bandia.
Akasema kada hizo pamoja wafanyakazi wa kampuni za mbegu walieleza kuwa takribani asilimia 20 ya mbegu zilizopo kwenye soko zina ubora hafifu unaoziweka katika kundi la pembejeo bandia.
Waliohojiwa katika utafiti huo, wamekaririwa wakieleza kuwa hali ya pembejeo bandia ni mbaya zaidi kwa upande wa viuatilifu. MAPENDEKEZO Utafiti huo unapendekeza, pamoja na mambo mengine, kuwapo mapitio yenye lengo la kuboresha mamlaka za usimamizi katika sekta ya kilimo, kuboresha uratibu miongoni mwa mamlaka hizo ili zifanye kazi zikilenga kuboresha huduma kwa mkulima na kumpunguzia gharama za uzalishaji.
Mapendekezo mengine ni kutangaza kwenye gazeti la serikali majina ya wakaguzi wa mbegu, mbolea na viuatilifu katika ngazi za wilaya na kuwajengea uwezo ili watimize wajibu wao kwa ufanisi.
Pia kufanikisha upatikanaji wa taarifa zinazohitajika katika kusajili, biashara na kuingiza pembejeo za kilimo. Kuongeza kiasi cha faini kwa wahusika wa pembejeo bandia na fidia kwa waathirika wa vitendo hivyo.
Mkurugenzi Mtendaji wa Baraza la Kilimo Tanzania (ACT), Janeth Bitegeko anasema mkutano wa kujadili matokeo ya utafiti huo ni jukwaa muhimu hasa katika kipindi hiki ambacho kasi ya utendaji kazi wa serikali ni kubwa, hivyo kuwapo uwezekano wa upungufu kadhaa kufanyiwa kazi tangu kufanyika kwa utafiti huo.
Bitegeko anasema kilimo ni biashara inayochangia maendeleo ya nchi, ustawi na uboreshaji huduma za jamii kutokana na fedha zinazopatikana kupitia kodi mbalimbali zinazotozwa kwenye sekta hiyo.
Ni kutokana na hali hiyo, Bitegeko anasema baraza limejikita katika kujenga uwezo wa wakulima na wadau wengine wa kilimo kuhusiana na mnyororo wa thamani ya mazao hususani katika kulima, kuvuna, kuuza na masoko

Wednesday, October 25, 2017

2019 World Economic Forum of Young Global Leaders – Call for Nominations

 

The WEF Forum of Young Global Leaders has established a comprehensive selection process for identifying and selecting the most exceptional leaders. Every year, thousands of candidates from around the world are proposed and assessed according to rigorous selection criteria. Only the very best candidates are selected and all efforts are extended to create a truly representative body. Reflecting the diversity of stakeholders, the Young Global Leaders include leaders from politics, business, civil society, academia, and arts and culture across seven geographic regions.

Selection Criteria:
· To be eligible for the Young Global Leaders Class of 2019, the candidate must have been born on or after 1 January, 1980.
· He/she has a recognized record of extraordinary achievement and a proven track record of substantial leadership experience. Typically, this means 5-15 years of outstanding professional work experience and a clear indication of playing a substantial leadership role for the rest of his or her career.
· He/she has demonstrated a personal commitment to serve society at large through exceptional contributions and a deep ethical fiber, and has earned significant trust at both local and global levels.
· He/she has an impeccable record in the public eye and good standing in his/her community, as well as show great self-awareness and a desire for learning.
· Candidates from the business sector must be responsible for the full operation of a qualifying corporation or division and must hold one of the following titles: President, Chairman of the Board, Chief Executive Officer, Managing Director, Managing Partner or Publisher, or equivalent of any of the above. If the company is a Member or Partner of the World Economic Forum, the candidate requires the approval of the CEO or Chairman of the Board of the respective company.
· Companies, organizations and entities can only nominate one candidate from the qualifying company every two years.
· Kindly note that self-nominations are not accepted.
Nomination and Selection Timeline
· 31 May: Close of nomination period
· Summer: The World Economic Forum shortlists candidates for further review
· Fall: The shortlisted candidates are reviewed by Heidrick & Struggles, recognised as one of the world’s leading executive search and leadership consulting firms
· Winter: A Selection Committee reviews the top candidates and selects 100 to be honoured as Young Global Leaders
· January of subsequent year: The candidates are informed of their selection as Young Global Leaders*
· March of subsequent year: The press announcement for the new Class of Young Global Leaders is released
* Due to the large number of nominations received, the World Economic Forum only contacts successful candidates regarding their selection to the Forum of Young Global Leaders. However, some candidates may be contacted as part of the due diligence process. 

For more Information follow the link below..
 https://www.weforum.org/pages/nominate-a-young-global-leader

TAMASHA LA 19 LA DUNIA LA VIJANA NA WANAFUNZI NCHINI URUSI



 

Vijana 28 kutoka Tanzania waliwakilisha nchi yetu katia tamasha la 19 la dunia la vijana na wanafunzi lililofanyika Sochi Urusi. Ni tamasha la 19 la Dunia la vijana na wanafunzi, ambalo limefanyika Sochi Urusi, kwa ambapo zaidi ya vijana 20,000 kutoka mataifa zaidi ya 184 walikutana kujadili maendeleo ya dunia kwa sasa na wakati ujao, pia kila nchi ilionesha utamaduni wao ikiwepo Tanzania. Suala zima ilikuwa ni kukutanisha vijana na wanafunzi kutoka ulimwengu wote kutafakari njia mpya za kutatua changamoto katika nchi zao na ulimwenguni.
Pia kujifunza jinsi Urusi ilivyo endelea kiviwanda, teknolojia, uongozi, utamaduni na kutazama upya mambo ya uchumi, kujitawala na kujitegemea na sio kunyonywa na mabepari au kutegemea misaada sana ambayo imeleta migogoro hasa nchi zinazoendelea.
Kingine ni kuona jinsi umoja wa mataifa unafanya kazi kwa kusimamia maazimio pia na kujadili changamoto zake.
Katika malengo ya ulimwengu SDGs tumeona ya UN yapo 17 lakini ya WFYS2017 tumeongeza 18 ambalo ni Technology as a way of innovations and sustainable development to any country (Putin aliiongelea hii sana). Mmoja kati ya watanzania (Peter Mmbando) yeye aliweza kuongelea amani za maziwa makuu na matumizi ya artificial intelligence katika kumaliza migogoro lakini mazungumzo ni njia sahihi
Baada ya Tamasha kuisha vijana walipat furs yauweza kutembelea baadhiya maeneo ambayo ni yakitalii lakini kikubwa walichokiona au kutembelea ni kuona viwanja vitakavyotumika katika kombe la dunia hapo mwakani 2018



































Kijana Peter akiwa katika mja ya viwanja vitakavyochezewakombe la dunia hapo mwakani 2018



kijana peter akibadilishana mawazo na Dr. Walter Schwimmer ambaye anahusika na maswala ya umoja wa mataifa na mambo ya amani