Wednesday, October 25, 2017

TAMASHA LA 19 LA DUNIA LA VIJANA NA WANAFUNZI NCHINI URUSI



 

Vijana 28 kutoka Tanzania waliwakilisha nchi yetu katia tamasha la 19 la dunia la vijana na wanafunzi lililofanyika Sochi Urusi. Ni tamasha la 19 la Dunia la vijana na wanafunzi, ambalo limefanyika Sochi Urusi, kwa ambapo zaidi ya vijana 20,000 kutoka mataifa zaidi ya 184 walikutana kujadili maendeleo ya dunia kwa sasa na wakati ujao, pia kila nchi ilionesha utamaduni wao ikiwepo Tanzania. Suala zima ilikuwa ni kukutanisha vijana na wanafunzi kutoka ulimwengu wote kutafakari njia mpya za kutatua changamoto katika nchi zao na ulimwenguni.
Pia kujifunza jinsi Urusi ilivyo endelea kiviwanda, teknolojia, uongozi, utamaduni na kutazama upya mambo ya uchumi, kujitawala na kujitegemea na sio kunyonywa na mabepari au kutegemea misaada sana ambayo imeleta migogoro hasa nchi zinazoendelea.
Kingine ni kuona jinsi umoja wa mataifa unafanya kazi kwa kusimamia maazimio pia na kujadili changamoto zake.
Katika malengo ya ulimwengu SDGs tumeona ya UN yapo 17 lakini ya WFYS2017 tumeongeza 18 ambalo ni Technology as a way of innovations and sustainable development to any country (Putin aliiongelea hii sana). Mmoja kati ya watanzania (Peter Mmbando) yeye aliweza kuongelea amani za maziwa makuu na matumizi ya artificial intelligence katika kumaliza migogoro lakini mazungumzo ni njia sahihi
Baada ya Tamasha kuisha vijana walipat furs yauweza kutembelea baadhiya maeneo ambayo ni yakitalii lakini kikubwa walichokiona au kutembelea ni kuona viwanja vitakavyotumika katika kombe la dunia hapo mwakani 2018



































Kijana Peter akiwa katika mja ya viwanja vitakavyochezewakombe la dunia hapo mwakani 2018



kijana peter akibadilishana mawazo na Dr. Walter Schwimmer ambaye anahusika na maswala ya umoja wa mataifa na mambo ya amani

0 comments:

Post a Comment