Tuesday, September 22, 2015

Unalifahamu bara la Africa? Haya ni mambo 25 kuhusu bara la Africa

Image result for africa

1 Bara la pili kwa ukubwa

Africa ni bara la pili kwa ukubwa miongoni mwa mabara saba ya Ulimwengu. Lina kilomita za mraba 30 million, kilomita 14 million pungufu ya bara linaloongoza kwa ukubwa; bara la Asia ambalo lina kilomita za mraba 44 million.

2 Kuna zaidi ya mapiramidi 220

Mapiramidi makubwa duniani hayapatikani nchini Misri, ila yanapatikana Sudan Kaskazini na Sudan Kusini. Kwa jumla nchi hizi zina mapiramidi zaidi ya 220, ambayo yanasadikiwa kuwa ni ya muda mrefu zaidi kuliko yale yanayopatikana nchini Misri.

3 Nchi inayoongoza kwa kuuza chai duniani inapatikana Afrika

Nchi inayoongoza kwa kuuza Chai Duniani inapatikana barani Africa. Ni nchi ya Kenya ambayo inaongoza kwa kuuza Chai nje ya nchi Duniani, pia ni miongoni mwa nchi zinazoongoza kwa kuuza maua nje ya nchi. Pia nchi za Libya, Angola, Algeria na Nigeria zote zimeingia katika 20 bora ya nchi zinazouza mafuta kwa wingi Duniani.

4 Idadi ya watu

Bara la Africa lina idadi ya watu wanaokadiriwa kufikia 1 billion.

5 Mto mrefu duniani

Mto mrefu duniani unapatikana barani Africa. Mto Nile ni mto mrefu zaidi duniani ambao una urefu wa kilomita 6,650. Pia mto Congo, ambao una urefu wa kilomita 4,700 unashika nafasi ya nane miongoni mwa mito mirefu duniani.

6 Nusu ya almasi zote duniani hutoka Afrika

Nusu ya almasi zote duniani, zinatoka kusini na Afrika ya kati.

7 Washindi 18 wa tuzo ya Nobel

Bara la Africa lina washindi 18 wa tuzo ya Nobel. Pia ni bara la pekee ambalo lina barabara ambayo washindi wawili wa tuzo ya Nobel wanaishi: mtaa wa Vilakazi mjini Soweto.

8 Chura mkubwa zaidi duniani

Chura mkubwa zaidi Duniani anapatikana barani Africa na amepatikana katika msitu wa nchi za Cameroon na Equatorial Guinea. Anaitwa Goliath, anaweza kukua na kufikia uregu wa mita moja na uzito wa kilo 3.

9 Jangwa kubwa

Jangwa la Sahara ambalo linapatikana barani Afrika, ni jangwa kubwa duniani. Kutokana na ukubwa wake, jangwa la Sahara limeenea katika nchi zipatazo 12, lina eneo kubwa kuliko bara la Ameraka ya Kaskazini.

10 Lagos yaongoza kwa idadi kubwa ya watu

Jiji linaloongoza kwa idadi kubwa ya watu barani Africa ni Lagos ambalo liko nchini Nigeria, lina jumla ya watu 7.9 million. Jiji la Kinshasa linalopatikana nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo ni la pili likiwa na jumla ya watu 7.8 million, wakati jiji la Cairo lililopo nchini Misri linashika namba tatu kwa kuwa na jumla ya watu 6.7 million.

11 Waanzilishi wa biashara ya kimataifa 

Wakati bara la Ulaya wanavamia Mashariki ya Kati wakati wa pita ya kwanza ya msalaba, muungano wa mito miwili ya Shashe na Limpopo ilikuwa makazi ya ufalme wa Mapungubwe. Himaya hii ilipatikana katika mpaka kati ya nchi za Zimbabwe, Botswana na Afrika Kusini, ambapo iliweza kufanya biashara kwa upana na mataifa mengi barani Afrika na hata ghuba ya Uarabuni.

12 Kila mmoja ana asili ya Afrika 

Kila mmoja ni Mwafrika kwa asili. Vipimo vya kisaba vya DNA vilivyofanywa vimethibitisha kuwa, binadamu wote ulimwenguni wanahusiana na watu wa kale ambao walihama barani Africa kiasi miaka 125,000 iliyopita. Watu wameanza kuzaliana zaidi katika mabara yote miaka 80,000 baada ya hapo.

13 Aina nyingi ya samaki

Ziwa Malawi, ambalo linachangiwa na nchi za Malawi, Msumbiji na Tanzania, linashika nafasi ya nane kwa ukubwa miongoni mwa maziwa duniani. Lakini ziwa ambalo linajivunia kuwa na aina ya samaki wanaopatikana sehemu yoyote duniani.

14 Nchi nyingi zaidi

Bara la lina jumla ya nchi 54; ni bara lenye nchi nyingi kuliko bara lolote. Bara la Asia, lina nchini 49.

15 Wanyama wa aina zote

Bara la Africa ni bara ambalo linapatikana wanyama wa aina zote yaani wenye kasi zaidi na wanyama wakubwa zaidi. Duma, ambaye anaweza kukimbia kwa umbali wa hadi kilomita 120 kwa saa, ni mnyama mwenye kasi zaidi duniani, wakati hakuna Tembo yeyote mkubwa zaidi ulimwenguni kuliko Tembo wa Africa.

16 Bonde kubwa la kijani

Mto wa samaki uliopo nchini Namibia unashika nafasi ya pili kwa kuwa na kina kirefu Ulimwenguni. Blyde River Canyon, nchini Afrika Kusini, ni mto ulio na bonde kubwa la kijani ulimwenguni.

17 Ghana ni nchi inayokuwa kiuchumi

Nchi ya Ghana ni nchi ya pili kwa ukuaji wa uchumi haraka ulimwenguni, ikitanguliwa na nchi ya Qatar.

18 Ziwa lenye kina kirefu

Ziwa Tanganyika lipatikanalo barani Africa, ni ziwa la pili kwa kuwa na kina kirefu ulimwenguni. Ziwa hili limekwenda chini kwa urefu wa zaidi ya kilomita 1.7. Hii ni pungufu ya mita 200 nyuma ya ziwa linaloongoza kwa kina kirefu ambalo linapatikana nchini Russia.

19 Lahaja 25%

Asilimia 25 ya lahaja zote ulimwenguni zinapatikana barani Africa. Nyingi ya lahaja hizi zinapatikana katikati na magharibi mwa Africa. Pia kuna karibu lugha tofauti 3,000 zinazozungumzwa barani Africa.

20 Kuba kubwa

Kuba Vredefort, lipatikanalo nchini afrika Kusini, linaoongoza ulimwenguni kwa ukubwa. Linapima kwa kilomita 300 kwa diameter – yaani kilomita 50 zaidi ya Kuba linaloshika namba mbili.

21 Binadamu ndugu wa kale wamegunduliwa Afrika

Binadamu wa kale ambao ni ndugu wamegundulika barani Africa. ‘Lucy’, miaka 3.2 million iliyopita, amegunduliwa nchini Ethiopia. ‘Ardi’, ambaye ni mzee wa kale aliyehangaika zaidi ya miaka 4.4 million iliyopita, amaegundulika karibu kilomita 50 kutoka alipogunduliwa Lucy.

22 Ziwa kubwa

Likiwa na kilomita za mraba 68,000, ziwa Victoria ni ziwa la pili kwa ukubwa ulimwenguni. Pia ni chanzo cha mto Nile.

23 Papa hatari 

Pwani ya kusini mwa Africa ni hatari sana kwa mashambulizi ya Papa. Hata hivyo nchi za Australia na Marekani zimeshuhudia mashambulizi zaidi, angalau 1/3 ya papa wa South Africa wanashambulia ambapo husababisha kifo.

24 Nchi yenye makabila mengi zaidi inapatikana Afrika 

Nchi ya Nigeria ina zaidi ya makabila yanayotambulika 370 na kutengana huku kukiwa na lugha hai 510. Kulinganisha, na bara la Ulaya likiwa pungufu kwa lugha 150 na nchi ya India ina lugha 400.

25 Limetengwa na mstari wa equatir

Africa ni bara pekee ambalo ni linatengwa na mstari wa equator. Nchi ya Afrika Kusini ni nchi pekee barani humu ambayo mstari huo umepita.

shudate blog

0 comments:

Post a Comment