Friday, August 21, 2015

KIPINDUPINDU DAR CHAOGOPESHA WATU HATA KUPEANA MIKONO

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Said Meck Sadik amewataka wakazi wa jijini hilo kuchukua hadhari za kiafya ikiwamo kuacha kusalimiana kwa kushikana mikono kutokana na mlipuko wa kipindupindu ambao mpaka sasa umeshawapata watu 56, kati yao watatu wamefariki dunia.

Akizungumza jana ofisini kwake, mbali na kushikana mikono, Sadik aliwataka wananchi kuacha kunywa maji ya viroba maarufu kama “maji ya Kandoro” na juisi za mitaani ili kupunguza uwezekano wa kupata ugonjwa huo.

“Masuala ya kusalimiana mikono kwa mikono katika kipindi hiki tuepukane nayo lazima tunyanyapaliane wakati huu, ndiyo maana nilipoingia hapa sikuwapeni mikono kwa sababu nazingatia masharti ya madaktari,” aliwaambia waandishi wa habari.

Alisema ugonjwa huo ulilipuka Agosti 15 baada ya mtu mmoja kufariki dunia katika Hospitali ya Mwananyamala. “Hata familia yake, mke na watoto walipochukuliwa vipimo na wao walidhihirika kwamba wana maambukizi ya kipindupindu na mpaka sasa hivi bado tunao katika kituo chetu cha afya pale Mburahati,” alisema Sadik.

Alisema idadi ya wagonjwa imeongezeka hadi kufikia 56 lakini mpaka sasa wamebaki wagonjwa 36 katika kituo maalumu kilichofunguliwa Mbagala baada ya wengine kutibiwa na kuruhusiwa kurudi nyumbani.

Aliwataka wananchi kuepuka kula chakula kilichopoa na matunda ambayo hayajaoshwa. Alizitaja dalili za za ugonjwa huo kuwa ni kuharisha mfululizo, choo kuwa cha majimaji meupe kama ya mchele, kutapika mfululizo, ngozi kusinyaa, kiu kali, mdomo kukauka, mapigo ya moyo kuongezeka na mwili kukosa nguvu.

Related Posts:

  • UEFA : MAN UNITED NA MAN CITY ZAANZA VIBAYA Timu za Uingereza za Man United na Man City zimeanza vibaya michuano ya kombe la klabu bigwa barani Ulaya baada ya kuchapwa. Man United wakiwa ugenini nchini Uholanzi wamelala kwa kichapo cha mabao 2-1 dhidi… Read More
  • VPL KUANZA HII LEO MSIMU 2015-16 MSIMU wa Ligi Kuu ya soka ya Tanzania Bara 2015-2016 unaanza leo kwa timu 14 kati ya 16 zikitarajiwa kushuka dimbani kuwania pointi tatu za kwanza. Timu zitakazoshiriki ligi hiyo inayochezwa kwa mtindo wa nyumbani na ugeni… Read More
  • HALI BADO NI NGUMU KWA WAKIMBIZI ULAYA Mamia ya wahamiaji wako katika hali ya sintofahamu katika eneo la mpaka wa Serbia na Hungary baada ya Serikali ya Hungary kufunga mpaka wake kwa uzio. Hatua hiyo inadhumuni la kuwazuia wahamiaji wanaojaribu kuingia katika… Read More
  • VPL LEO INAENDELEA Ligi Kuu Tanzania bara Itaendelea tena leo katika viwanja saba ikiwa ni michezo ya mzunguko wa pili. Mabingwa watetezi wa kombe hilo klabu ya Young Africans watakuwa wenyeji wa Tanzania Prisons katika uwanja wa Taifa jijin… Read More
  • Mataifa ya Ulaya kujadili suala la wakimbizi Mawaziri wa mambo ya nchi za nje wa Ujerumani na Luxembourg wanatarajia kukutana na wenzao wa Jamuhuri ya Czech, Hungary, Poland na Slovakia mjini Prague kwa ajili ya kujadili suala la wakimbizi. Rais wa Halimashauri ya um… Read More

0 comments:

Post a Comment