Thursday, August 20, 2015

LORI LILILONASWA LIKISAFIRISHA WAHAMIAJI LILIIBWA NCHINI KENYA

Lori lenye usajili wa serikali ya Kenya, GK lilokuwa likisafirisha raia wa Ethiopia karibu 100 liliposhikwa na polisi katika eneo la Kangeta, Kaunti ya Meru Agosti 18, 2015. Picha/DAVID MUCHUI

Kamishna wa polisi Kaunti ya Marsabit Bw Peter Thuku alielezea Taifa Leo kuwa lori hilo lilikuwa la kundi la kukabiliana na wizi wa mifugo na halikupewa idhini la kutoka kambini.
Bw Thuku alikanusha madai kuwa dereva wa lori hilo aliyetoroka alikuwa polisi.
Aliongeza kuwa afisa wa polisi William Kipchirchir aliyenaswa na kupelekwa Kortini eneo la Maua kaunti ya Meru alitumia raia kuendesha lori hilo.
Bw Thuku alitibitisha kuwa dereva wa lori hilo alikuwa likizo.
Alisema kuwa lori hilo lilitumia barabara la kutoka Kaunti ya Wajir likapitia vichakani kabla ya kuingia Kaunti ya Isiolo na Meru.
“Afisa huyo amekiuka sheria. Tunashangaa kuwa afisa wa polisi anaeza toroka na gari la kituo cha polisi. Alitumia njia ambalo halikuwa na maafisa wa polisi. Hii ni uhalifu na sheria lazima ichukue mkondo wake,” alisema.
Alikashifu kisa hicho akidai kuwa ni utumiaji mbaya wa gari la serikali. Aliongeza kuwa kushikwa kwa askari wa polisi huyo inafaa iwe funzo kwa wengine wote.
“Nimefurahi alishikwa kabla ya kutimiza lengo lake,” Bw Thuku alisema

Kamishana huyo alidai kuwa wakimbizi wamekwepa kutumia barabara ya Marsabit kwa maana kuna maafisa wa polisi wengi anbao wameshika doria.
Kukwepa maafisa wa trafiki
Gari la polisi lilinaswa Kangeta katika Kaunti ya Meru Jumanne lilipojaribu kukwepa maafisa wa trafiki huku likiwa limebeba raia wa Ethiopia.
Mkazi mmoja aliwajulisha maafisa wa polisi kabla ya gari hilo kuzuiliwa.
Raia hao waliojificha ndani ya hema iliyotumiwa kufunika lori hilo, walisema walikuwa wanaelekea Afrika Kusini kutafuka kazi.
Raia hao wa Ethiopia 78 walifikishwa Kortini na kufungwa kwa miezi mitatu and kuachiliwa kwa dhamana ya Sh50,000 kila mmoja kabla ya kurudishwa nchini kwao. Wawili wao hawakuweza kufika mahakamani kwa kuwa walikuwa wagonjwa.
Kipchirchir, alikana madai ya kusafirisha raia wa Ethiopia kutumia gari la serikali kinyume na sheria na akazuiliwa katika kituo cha polisi hadi Agosti 21.

0 comments:

Post a Comment