Friday, September 4, 2015

ESRF: MABADILIKO YA KISERA YATAKUZA VIWANDA VIDOGO VIDOGO (SIDO)



SERIKALI imetakiwa kufanya mabadiliko makubwa ya kisera kuwezesha kukua kwa viwanda vidogo na vya kati nchini.
Kauli hiyo imo katika utafiti uliofanywa na Taasisi ya Utafiti wa Uchumi na Jamii (ESRF) kuhusu ukuaji wa sekta hiyo katika muktadha wa upatikanaji wa fedha.
Akiwasilisha utafiti huo mmoja wa watafiti, Hossana Mpango alisema kwamba kwenye utafiti wao wamebaini mgongano mkubwa wa kisera na utendaji, unaosababisha kukwama kwa maendeleo ya sekta hiyo.
Alisema ingawa kuna tatizo kubwa la ajira ambalo limefanya watu wengi kukimbilia kujiajiri wenyewe, kuna changamoto kubwa katika sekta hiyo hasa sera na uwapo wa mlolongo wa taasisi zinazopishana mamlaka na huku wakiwa ndio wanatoa leseni wachukua tozo.
Alizitaja taasisi hizo zinazopishana mamlaka kama Shirika la Viwango nchini (TBS), Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA), Mamlaka ya Mapato (TRA) halmashauri mbalimbali.
Alisema mabadiliko ya kisera yatawezesha kutengeneza muundo unaojali ukuaji wa sekta hiyo hasa kwa kuangalia kodi zinazolipwa ambazo kwa sasa ni za aina moja bila kuangalia uwekezaji unaohusika.
Alisema mabadiliko ya kisera yatasaidia kuimarisha sheria na kuweka sawa mwelekeo wa sekta hiyo kwa kuzingatia kwamba inahitaji mchango mkubwa wa nje wa kifedha ili kukua.
Pia utafiti huo ulishauri kwamba serikali ni lazima kutenga fungu ambalo litatumiwa na taasisi kama SIDO, NEEC na hata maofisa biashara wa wilaya kwa ajili ya mafunzo ya uajasiriamali na uendeshaji wa biashara.
Mapema Mkuu wa idara ya utafiti na machapisho wa ESRF, Profesa Fortunata Makene aliwataka washiriki wa warsha hiyo kutoa michango katika kuboresha uelewa ili serikali iweze kutatua kizungumkuti cha ukuaji wa sekta hiyo.
 SHUDATE BLOG

Related Posts:

  • WANAJESHI WA CAMEROON WASITISHA MGOMO Wanajeshi wa Cameroon, ambao wamekuwa kwenye mgomo baridi, kulalamikia kutolipwa mishahara yao, baada ya kuhudumu katika kikosi cha Umoja wa Mataifa, katika Jamuhuri ya Afrika ya Kati, wamesitisha mgomo. Image copyrightAFPIm… Read More
  • Mataifa ya Ulaya kujadili suala la wakimbizi Mawaziri wa mambo ya nchi za nje wa Ujerumani na Luxembourg wanatarajia kukutana na wenzao wa Jamuhuri ya Czech, Hungary, Poland na Slovakia mjini Prague kwa ajili ya kujadili suala la wakimbizi. Rais wa Halimashauri ya um… Read More
  • Ayew mechazaji bora Uingereza Mshambulizi matata wa klabu ya Swansea City Andre Ayew, ameteuliwa kuwa mchezaji bora wa mwezi uliopita, katika ligi kuu ya Uingereza ya Premier Nahodha huyo wa timu ya taifa ya Ghana mwenye umri wa miaka 25, amefunga mago… Read More
  • Mlipuko mkubwa watokea Yola, AdamawaImage copyrightAPImage captionMaafisa wa shirika la msalaba mwekundu Yola Mlipuko mkubwa umetokea katika kambi moja ya wakimbizi wa ndani, mjini Yola, mji mkuu wa Jimbo la Kaskazini Mashariki la Adamawa. Mashirika ya kutoa m… Read More
  • EMPLOYMENT OPPORTUNITY 1. MEDICAL OFFICER II (5 POSITIONS) Reports to : Head of Firm Duties and Responsibilities • To perform Medical duties in Obstetrics and Gynaecology, Surgery,Anaesthesia Medicine, Paediatrics, Preventive Medicine and … Read More

0 comments:

Post a Comment