Thursday, September 3, 2015

Wanajeshi 50 wa AU wauawa Somalia



Takriban wanajeshi 50, wa kutunza amani wa Muungano wa Afrika, wengi wao kutoka Uganda, wanasadikika kuuawa kwenye shambulio, lililofanywa siku ya Jumanne na wapiganaji wa Al shabaab, katika kambi ya Jannale, ulioko umbali wa kilomita 115 Kusini mwa mji mkuu wa Somalia, Mogadishu.
Wakaazi wa wilaya hiyo wamethibitisha kuwa kambi hiyo ilishambuliwa na wapiganaji hao wa Al Shabaab.
Wanasema wameonya helicopta za kijeshi mapema hii leo ikiwatafuta wanajeshi waliopotea katika maeneo ya mashambani na pia kuwauliza wakaazi hao ikiwa wamewaona wanajeshi wa AU wakiwa hai au wakiwa wameuawa.
Miili tatu ilipatikana karibu na kijiji hicho, baada ya watu hao kuzama ndani ya mto wakati wa makabiliano makali ya risasi.
Wanasema kuwa waliwapata wanajeshi kadhaa wakiwa hai na wengine wakiwa wameuawa.
Wanajeshi hao wa AU wanakabiliwa na wakati mgumu katika operesheni hiyo kwa sababu daraja inayounganisha mji huo uliharibiwa kwa mabomu hiyo jana.
Hali imeanza kutulia mjini humo lakini wakaazi wanaamini kuwa zaidi ya wanajeshi 40 hawajulikani waliko.
Makao makuu ya kikosi cha Muungano wa Afrika nchini Somalia, AMISOM, imethibitisha kuwa waliwapoteza wanajeshi akdhaa kutoka Uganda lakini idadi yao haijulikani.
SHUDATE BLOG

0 comments:

Post a Comment