Thursday, September 3, 2015

Wanajeshi 50 wa AU wauawa Somalia



Takriban wanajeshi 50, wa kutunza amani wa Muungano wa Afrika, wengi wao kutoka Uganda, wanasadikika kuuawa kwenye shambulio, lililofanywa siku ya Jumanne na wapiganaji wa Al shabaab, katika kambi ya Jannale, ulioko umbali wa kilomita 115 Kusini mwa mji mkuu wa Somalia, Mogadishu.
Wakaazi wa wilaya hiyo wamethibitisha kuwa kambi hiyo ilishambuliwa na wapiganaji hao wa Al Shabaab.
Wanasema wameonya helicopta za kijeshi mapema hii leo ikiwatafuta wanajeshi waliopotea katika maeneo ya mashambani na pia kuwauliza wakaazi hao ikiwa wamewaona wanajeshi wa AU wakiwa hai au wakiwa wameuawa.
Miili tatu ilipatikana karibu na kijiji hicho, baada ya watu hao kuzama ndani ya mto wakati wa makabiliano makali ya risasi.
Wanasema kuwa waliwapata wanajeshi kadhaa wakiwa hai na wengine wakiwa wameuawa.
Wanajeshi hao wa AU wanakabiliwa na wakati mgumu katika operesheni hiyo kwa sababu daraja inayounganisha mji huo uliharibiwa kwa mabomu hiyo jana.
Hali imeanza kutulia mjini humo lakini wakaazi wanaamini kuwa zaidi ya wanajeshi 40 hawajulikani waliko.
Makao makuu ya kikosi cha Muungano wa Afrika nchini Somalia, AMISOM, imethibitisha kuwa waliwapoteza wanajeshi akdhaa kutoka Uganda lakini idadi yao haijulikani.
SHUDATE BLOG

Related Posts:

  • OTAMENDI ATUA CITY Manchester City wamemsajili beki Nicolas Otamendi kutoka Valencia kwa mkataba wa miaka mitano wenye thamani ya pauni milioni 32. City watalipa kwanza pauni milioni 28.5 kumpata mchezaji huyo wa kimataifa wa Argentina amb… Read More
  • MGOMBEA URAISI KUPITIA CHAMA CHA ACT- WAZALENDO Hatimaye Chama cha ACT – Wazalendo kimempitisha mwenyekiti wake, Anna Mghwira (56) kuwania urais baada ya mshauri wake, Profesa Kitila Mkumbo aliyekuwa amechukuliwa fomu kukataa kubeba jukumu hilo. Sambamba na Mghwir… Read More
  • MGOMBEA UBUNGE CHADEMA ATEKWA Mgombea ubunge jimbo la Shinyanga mjini na m/kiti BAVICHA Taifa, ndugu Patrobas Katambi inasemekana ametekwa muda mfupi uliopita na kunyang'anywa fomu zake za ubunge. Nimezungumza na mwenezi wa jimbo hilo na kuthibitisha h… Read More
  • KIPINDUPINDU DAR CHAOGOPESHA WATU HATA KUPEANA MIKONO Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Said Meck Sadik amewataka wakazi wa jijini hilo kuchukua hadhari za kiafya ikiwamo kuacha kusalimiana kwa kushikana mikono kutokana na mlipuko wa kipindupindu ambao mpaka sasa umeshawapat… Read More
  • Mabadiliko ya Terehe ya Mitihani ya Marudio na Mitihani Maalum MABADILIKO YA TAREHE YA MITIHANI YA MARUDIO NA MITIHANI MAALUM (SUPPLEMENTARY/SPECIAL EXAMINATIONS) ILIYOKUWA IFANYIKE TAREHE 24 - 28/08/2015 Chuo Kikuu cha Dodoma kinawatangazia wanafunzi wote wa mwaka wa mwisho wa … Read More

0 comments:

Post a Comment