Friday, September 11, 2015

Mlipuko mkubwa watokea Yola, Adamawa

Image copyrightAP
Image captionMaafisa wa shirika la msalaba mwekundu Yola
Mlipuko mkubwa umetokea katika kambi moja ya wakimbizi wa ndani, mjini Yola, mji mkuu wa Jimbo la Kaskazini Mashariki la Adamawa.
Mashirika ya kutoa misaada ya dharura yamethibitisha mlipuko huo na kusema kuwa maafisa wa polisi wameuzingira eneo hilo kwa sasa.
Image copyrightGetty
Image captionRaia waliojeruhiwa
Mlipuko huo ulitokea katika chumba kimoja cha kuhifadhi vyakula katika kambi ya Malkohi.
Haijabainika nini kilisababisha mlipuko huo na ni wakimbizi wangapi wameathirika.
Ripoti zinasema kuwa zaidi ya watoto 1000 walikuwa katika kambi hiyo, iliyojengwa kuwahifadhi watu waliokimbia makwao kutokana na uasi unaoendelea Kaskazini Mashariki mwa Nigeria.
Maafisa wa shughuli za uokozi wametumwa katika eneo hilo huku uchunguzi ukiendelea.
Image copyrightAP
Image captionEneo la mkasa limezingirwa na maafisa wa polisi huku uchunguzi ukiendelea

Related Posts:

  • KAMA UNAHITAJI SCHOLARSHIP HEBU PITA HAPA COMMONWEALTH SCHOLARSHIPS TENABLE IN SOUTH AFRICA COMMONWEALTH SCHOLARSHIPS TENABLE IN SOUTH AFRICA.pdf Download Details Scholarship Tenable in Peoples Friendship University of Russia Scholarship Te… Read More
  • Swaziland yasema waliokufa kwenye ajali ni 13 tu Kinyume na taarifa zilizotolewa, serikali ya Swaziland inasema ni watu 13 tu waliopoteza maisha kwenye ajali ya barabarani iliyohusisha wanawake na wasichana waliokuwa wakielekea kwenye tamasha la densi. Taarifa hiyo ime… Read More
  • UDOM STRATEGIC PLAN HII HAPA UDOM Strategic Plan UDOM STARTEGIC PLAN 2012/2013 - 2016/2017 PDF                                         &… Read More
  • AJIRA CHUO KIKUU CHA DODOMA Academic Staff academic - 2015.pdf Download Details Administrative Staff administrative - 2015.pdf Download Details Employment Referee's Form Employment Referee's Form.pdf … Read More
  • Segun Odegbami ametangaza nia ya uraisi FIFA Mchezaji wa zamani wa timu ya taifa ya Nigeria Segun Odegbami ametangaza nia ya kuwania kiti cha urais katika chama cha soka duniani FIFA. Segun mwenye miaka 63 Alitwaa kombe la mataifa ya Afrika mwaka 1980 aikwa mchezaji… Read More

0 comments:

Post a Comment