Friday, September 11, 2015

KUELEKEA MECHI YA MAN VS LIVERPOOL : STEVEN GERRARD ASEMA NINGEBAKI ANFIELD KAMA NIPEWA OFA HII.

gerrard

Kuelekea kwenye mechi muhimu ambayo Liverpool wanayo dhidi ya Manchester united Jumamosi hii, lazima watamkumbuka captain wao Steven Gerrard. Captain wao alikua na uzoefu uwanjani, anaongoza kwa mfano akicheza kwa nguvu zote ili timu ishinde. Lakini kwa sasa hayupo tena na mechi itachezwa kama kawaida na wanaitaji ushindi bila ya yeye kuwepo.
Steven Gerrard amesema kwamba angeweza kubaki Liverpool kama angepata ofa ya tofauti kidogo. Kuna wakati mchezaji kama yeye anahitaji zaidi ya mkataba mpya wa pesa. Gerrard anasema “Nilishangazwa kwanini wakati wa mazungumzo na agent wangu, cheif executive wa club hakutaja majukumu ya kumsaidia kocha lakini labda itatokea siku moja. Nimekaa kama mchezaji kwenye timu kwa muda nikiongoza wenzangu, labda ningepata nafasi ya kujifunza zaidi kuhusu ukocha na management ingekua kitu cha ziada kwangu. Niliondoka wakati milango ipo wazi lakini bado ingewezekana kuwa Liverpool sasa hivi. Lakini kwanini Liverpool isingenifanyia mimi kama Manchester ilivyomfanyia Ryan Giggs”
Pia Gerrard anakubali kwamba amei-miss ligi ya kwao England,“Ndio nai-misss sana, na miss kila kitu kuhusu EPL. Naangalia TV kuona mechi zikiwa na mashabiki elfu 50, 60 hadi 70. Hali na ushindani kuhusu hilo nakubali kuwa namiss sana EPL”.Steven Gerrard anajiandaa kutoa kitabu chake ambacho amezungumza mambo mengi kuhusu maisha yake ya soka hadi anahamia ligi ya Marekani.

Related Posts:

  • ZIJUE FAIDA ZA TANGO Mwili wa binadamu ili uweze kuwa katika afya nzuri, unahitaji kuwa na virutubisho vya kutosha. Virutubisho hivi tunavipata katika vyakula, matunda na hata kupitia katika vinywaji mbalimbali tunaweza kupata vitu muhimu kwa a… Read More
  • LIST YA MAREFA WATAKAOCHEZESHA VPL WAAMUZI WA LIGI KUU YA VODACOMKamati ya Waamuzi nchini imetangaza orodha ya waamuzi wanaotakiwa kushiriki Semina na mtihani wa waamuzi itakayoanza tarehe 21- 25 Agosti, 2015 jijini Dar es salam, Waamuzi hao na sehemu wanaoz… Read More
  • FAIDA YA ASALI ASALI inafahamika kwa muda mrefu kama chakula muhimu ambacho pia kinasaidia sana katika kupambana na magonjwa mbalimbali na matatizo yatokanayo na uzee. Kwa mujibu wa tafiti mpya za wataalamu wa madawa lishe na vifaa tiba, … Read More
  • ZIJUE FAIDA 10 ZA TENDE Katika mwezi mtukufu wa Ramadhani, tende ndiyo tunda linaloliwa kwa wingi, pengine kuliko tunda lingine. Pamoja na kuwa ni tunda lenye ladha tamu na nzuri mdomoni, lakini kisayansi pia limethibitika kusheheni madini na vi… Read More
  • TIKETI ZA VISHINA KUENDELEA KUTUMIKA VPL 2015/16 Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) limeendelea kujiaibisha baada ya jana kueleza kuwa litatumia tiketi za mfumo wa kizamani za vishina kwenye mechi za Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara (VPL) msimu huu.Msimu huu wa ligi hiyo … Read More

0 comments:

Post a Comment