Wednesday, September 9, 2015

SIMBA FC KUELEKEA TANGA SIKU YA LEO KUTAFUTA POINT ZA LIGI TA VPL INAYOTARAJIWA KUANZA JUMAMOSI HII

Image result for simba fc

KIKOSI cha Simba kinatarajia kuondoka leo kwenda Tanga kwa ajili ya mechi ya ufunguzi wa Ligi Kuu Tanzania Bara inayotarajiwa kuanza Jumamosi dhidi ya African Sports ya huko.
Simba ilipiga kambi Zanzibar kwa maandalizi ya ligi hiyo kwa takribani wiki mbili zilizopita. Msemaji wa Simba, Haji Manara alisema jana kikosi chake kipo tayari kuanza ligi.
“Timu imemaliza rasmi kambi yake Zanzibar na kesho (leo) itafanya safari ya kwenda Tanga, tunatarajia kupata matokeo mazuri kwenye mechi hiyo,” alisema.
Simba inasaka ubingwa kwa udi na uvumba baada ya kuukosa kwa zaidi ya misimu mitatu. Kocha Mkuu wa timu hiyo, Dylan Kerr alisema ana imani timu yake itaibuka na ushindi katika mechi hiyo ya kwanza na ile ya pili dhidi ya Mgambo Shooting itakayochezwa Septemba 16 huko huko Tanga.
Kerr ameifuatilia African Sports ikicheza mechi ya kirafiki na Coastal Union mwishoni mwa wiki iliyopita na kusema hashindwi kuifunga. Simba baada ya kucheza na African Sports, itashuka dimbani kwenye uwanja huo kucheza na Mgambo JKT Jumatano ijayo.
Kerr alisema lengo lake ni kushinda mechi hiyo ili kuwaondoa woga wachezaji wake katika mechi zijazo.
“Kwenye soka unapoanza vizuri mechi ya kwanza unajijenga kujiamini mechi zijazo, utashinda ya pili na ya tatu na kuendelea na mwisho kutwaa ubingwa, nataka kushinda mechi ya kwanza kuwafanya wachezaji wangu wajiamini,” alisema.

Related Posts:

  • JK: Ndoto kuipaisha Kigoma zinatimia RAIS Jakaya Kikwete amesema ndoto yake ya kuuona mkoa wa Kigoma ukileta mabadiliko makubwa ya kiuchumi nchini imeanza kutimia, kutokana na kuanza kutekelezwa kwa miradi mbalimbali ya kiuchumi. Aidha, amewahakikishia wanan… Read More
  • Ghasia zaendelea kwenye eneo la Msikiti wa Al-Aqsa Leo ni siku ya tatu tangu mapambano yaanze baina ya polisi na Waislamu kwenye eneo la msikiti wa Al-Aqsa Kwa mujibu wa taarifa kutoka ofisi ya Rais, Bwana Erdogan amemwambia Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa,Ban Ki-moon kwa … Read More
  • VPL LEO INAENDELEA Ligi Kuu Tanzania bara Itaendelea tena leo katika viwanja saba ikiwa ni michezo ya mzunguko wa pili. Mabingwa watetezi wa kombe hilo klabu ya Young Africans watakuwa wenyeji wa Tanzania Prisons katika uwanja wa Taifa jijin… Read More
  • Merkel aitisha mkutano kujadili mgogoro wa wakimbizi Kansela wa Ujerumani Angela Merkel ameitisha mkutano wa kilele wa Umoja wa Ulaya wiki ijayo kuhusu mgogoro wa wakimbizi, akisema suluhu ya pamoja inahitajika ili kukabiliana na mgogoro huo uliyougawa Umoja wa Ulaya. Kansel… Read More
  • Mafuriko Nyumba ya Mungu yasomba ekari 20 ZAIDI ya ekari 20 za mazao ya aina mbalimbali, ikiwamo vitunguu na mahindi pamoja na nyumba ambazo idadi yake haijulikani katika vijiji vya Jitengeni na Mvungwe wilayani Same, zimeharibiwa na mafuriko kutoka bwawa la Nyumb… Read More

0 comments:

Post a Comment