Friday, September 4, 2015

Mwanajeshi wa Uholanzi ajiunga na Islamic state



Mwanajeshi wa jeshi la wanahewa la Uholanzi, anadaiwa kusafiri hadi nchini Syria na kujiunga na kundi la wapiganaji la Islamic State.
Wizara ya ulinzi ya Uholanzi, imesema mwanajeshi huyo ni sajini wa umri mwenye umri wa miaka 26.
Maafisa nchini humo, bado wanaendelea kuchunguza ikiwa kuna mafunzo ya itikadi kali ndani ya jeshi la Uholanzi.
Iwapo tuhuma hizo zitathibitishwa, basi itakuwa mara ya kwanza kwa mwanajeshi anayehudumu katika jeshi la Uholanzi kwenda kujiunga na Islamic State.
Kupitia taarifa wizara ya ulinzi ilisema sajini huyo, amefukuzwa jeshini na hawezi tena kupokea habari za kijasusi za jeshi.
Huwa ni kosa la jinai nchini Uholanzi kwa raia kusafiri ng'ambo kujiunga na IS.
Waholanzi takriban 180, wanaaminika kuondoka taifa hilo na kujiunga na makundi ya wapiganaji Iraq na Syria.
Waziri wa Ulinzi wa Uholanzi, Jeanine Hennis Plasschaert, amesema litakuwa ni jambo la "kusikitisha" ikibainika kwamba mwanamume mmoja "ameungana na waovu" wenzake kwenye jeshi "wanahatarisha maisha kulinda haki na uhuru wa watu wengine."
SHUDATE BLOG

Related Posts:

  • UEFA : MAN UNITED NA MAN CITY ZAANZA VIBAYA Timu za Uingereza za Man United na Man City zimeanza vibaya michuano ya kombe la klabu bigwa barani Ulaya baada ya kuchapwa. Man United wakiwa ugenini nchini Uholanzi wamelala kwa kichapo cha mabao 2-1 dhidi… Read More
  • VPL LEO INAENDELEA Ligi Kuu Tanzania bara Itaendelea tena leo katika viwanja saba ikiwa ni michezo ya mzunguko wa pili. Mabingwa watetezi wa kombe hilo klabu ya Young Africans watakuwa wenyeji wa Tanzania Prisons katika uwanja wa Taifa jijin… Read More
  • Ghasia zaendelea kwenye eneo la Msikiti wa Al-Aqsa Leo ni siku ya tatu tangu mapambano yaanze baina ya polisi na Waislamu kwenye eneo la msikiti wa Al-Aqsa Kwa mujibu wa taarifa kutoka ofisi ya Rais, Bwana Erdogan amemwambia Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa,Ban Ki-moon kwa … Read More
  • HALI BADO NI NGUMU KWA WAKIMBIZI ULAYA Mamia ya wahamiaji wako katika hali ya sintofahamu katika eneo la mpaka wa Serbia na Hungary baada ya Serikali ya Hungary kufunga mpaka wake kwa uzio. Hatua hiyo inadhumuni la kuwazuia wahamiaji wanaojaribu kuingia katika… Read More
  • Merkel aitisha mkutano kujadili mgogoro wa wakimbizi Kansela wa Ujerumani Angela Merkel ameitisha mkutano wa kilele wa Umoja wa Ulaya wiki ijayo kuhusu mgogoro wa wakimbizi, akisema suluhu ya pamoja inahitajika ili kukabiliana na mgogoro huo uliyougawa Umoja wa Ulaya. Kansel… Read More

0 comments:

Post a Comment